Monday 28 March 2016

WATALAM WAELEKEKEZI KUTOKA SAGCOT WAKUTANA NA WATAALAM WA WIZARA

Mkurugenzi wa Sera na Mipango Bw. James Lugaganya (wakwanza kushoto) akiwa na wataalam waelekezi kutoka SAGCOT  katika Mkutano uliofanyika jengo la Waterfront Jijini Dar
Wataalam waelekezi kutoka SAGCOT (kulia) wakiwa na wataalam wa Wizara Bw. Mashaka Chikoli (wapili kulia) na Bw. Juvenal Lema (wakwanza kulia) wakiwa kwenye Mkutano uliofanyika  katika Jengo la Waterfront Jijini Dar es Salaam

Friday 18 March 2016

BUNGE LA EALA KUWAENZI WAKE WA WAASISI WA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI

Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki (EALA) limepitisha kwa sauti moja hoja ya kuwaenzi wake wa Marais Waasisi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki iliyopita (1967-77), wake hao ni Mama Maria Nyerere (Tanzania), Mama Ngina Kenyata(Kenya) na Mama Mirium Obote (Uganda).
 Hoja hii iliwasilishwa Bungeni na Mhe. Mumbi Ng’aru kutoka Kenya, hoja hii wakati ikiwaslishwa ilivuta hisia za wabunge wengi, akiongea wakati anawasilisha hoja hiyo aliomba Bunge kuunga mkono hoja hiyo na kuwaalika katika kikao cha Bunge kinachotarajiwa kufanyika Mei, 2016 Jijini Arusha.

Akiongea wakati anawailisha hoja hiyo alisema wakati umefika sasa Bunge kutambua mchango wa wakina mama hawa wanaobeba historia kubwa ya Jumuiya, kwani wakati Marais hawa wanahangaika na harakati za kuunganisha nchi za Afrika Mashariki wao walikuwa bega kwa bega na Marais hawa kuwasaidia hasa katika kuwashauri vizuri na kuaangalia familia, huu ni ukweli usioweza kufumbiwa macho, kwani akina mama hawa wameendelea kutoa mchango wao kwa Mataifa yetu na Jumuiya yetu ya sasa kwa kutoa viongozi ambao wanaitumikia Nchi zetu na Jumuiya yetu kwa namna moja au nyingine.

“Nilibahatika kuzungumza na akina mama hawa kwa nyakati tofauti, na kwa kweli akina mama hawa ni zaidi ya maktaba ya masuala ya Afrika Mashariki, ni hadhina ambayo tuna kila sababu ya kujivunia” alisema Mhe. Mumbi. Wabunge kwa sauti moja walikubaliana akina mama hawa kualikwa katika Kikao cha Bunge kitakachofanyika Arusha na kuhutubia Bunge hilo.

Wabunge wengine waliochangia hoja hii kutoka Tanzania ni Mhe. Shyrose Bhanji, Mhe. Makongoro Nyerere na Mhe. Nderakindo Kessy.

Katika hatua nyingine Bunge limepitisha ripoti ya Kamati ya Masuala ya Sheria, ripoti hiyo iliyohusu uoanishaji na uhuishaji wa Sheria za ndani ya Nchi wanachama na zile za Jumuiya, akichangia wakati wa majadiliano kuhusu ripoti hii Mhe. Abdullah Mwinyi alisema utekelezaji wa hatua mbalimbali za Mtangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki hasa umoja wa forodha na Soko la Pamoja utategemea zaidi kuhuishwa kwa sheria hizi kwani sheria nyingi za Nchi wanachama zinakinzana na zile za Jumuiya hivyo kufanya utekelezaji kuwa mgumu na wanaoathirika zaidi ni wananchi ambao ndio watumiaji wa sheria hizo.


Bunge hili lilianza vikao vyake tarehe 7 Machi,2016 na kukamilisha Vikao vyake Jana tarehe 17 Machi, 2016, pamoja na mambo mengine Musuada wa kuzuia usafirishaji haramu wa binadamu (EAC Counter Trafficking in Persons Bill,2016), ulisomwa kwa mara ya kwanza.

Wednesday 9 March 2016

WAZIRI MKUU MHE. KASSIM MAJALIWA AHUTUBIA BUNGE LA AFRIKA MASHARIKI (EALA)

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa (wakwanza kushoto) akiwasili katika ukumbi wa Mikutano wa Benki Kuu ya Tanzania ambapo alitoa hotuba ya ufunguzi wa mkutano wa 5 wa Bunge la 3 la Jumuiya ya Afrika Mashariki unaoendelea Jijini Dar. Alioambatana nao ni Spika wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki Mhe. Job Ndugai, (aliyetangulia mbele) Spika wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki Mhe. Daniel Kidega (katikati) na Katibu Mkuu wa Sekretariati ya Jumuiya ya Afrika Mashariki Balozi Dkt. Richard Sezibera. Mkutano huu uatafanyika kwa siku 12 kuanzia Machi 6-18, 2016
Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa (watatu kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Waheshiwa Wabunge. 
Waziri Mkuu Mhe. Kassim Mjaliwa akijadili jambo na Spika wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki Mhe. Daniel Kidega mara baada ya kuahirishwa kwa Mkutano wa Bunge hilo.
Waheshimiwa Wabunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki wakiendelea Mkutano.
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai akihutubia Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki Machi 8, 2016.
Waziri Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (kushoto) akifuatilia Mkutano wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki. Mhe. Balozi Dkt. Mahiga pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Waziri Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akila kiapo kwa mujibu wa sheria ili awezekushiriki katika Mkutano wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki Machi 8, 2016
Waziri Mkuu Mhe. Kassim Mjaliwa akitoa hotuba ya ufunguzi wa Mkutano wa 5 wa Bunge la 3 la Afrika Mashariki katika ukumbi wa Mikutano wa Benki Kuu ya Tanzania Jijini Dar Machi 8, 2016
Tokea kushoto; Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, Spika wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki Mhe. Daniel Kidega na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai wakishiriki kuimba na kutoa heshima wakati wimbo wa Taifa ukiibwa.
Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akimsiliza Spika wa Bunge la Afrika Mashariki Mhe. Daniel Kidega Machi 
Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akisaini kitabu cha wageni kabla ya kutoa hotuba ya ufunguzi wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki linaloendelea na Mkutano wake Jijini Dar, kulia ni Spika wa Bunge hilo Mhe. Daniel Kidega.

Sunday 6 March 2016

AFRIKA MASHARIKI YAZINDUA EAST AFRICAN COMMUNITY APP

DOWNLOAD YOUR FAVORITE EAST AFRICAN COMMUNITY APP 
Pakua kutoka simu yako ya mkononi ujipatie taarifa mbalimbali kuhusu Jumuiya ya Afrika Mashariki. Kupitia hii utapata kuona takwimu mbalimbali, fursa za biashara na ajira.

HABARI PICHA; MAKAMU WA RAIS AFUNGUA SEMINA YA 9 YA WABUNGE WA EALA NA WABUNGE WA NCHI WANACHAMA

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluh Hassan (wakwanza kulia) akitoa hotuba ya Ufunguzi wa Semina ya 9 ya kuimarisha uhusiano (Nanyuki 9) kati ya Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki na Wabunge kutoka Nchi Wanachama. Semina hii hufanyika kila mwaka kwa mzunguko katika Nchi Wanachama na kwa mara ya kwanza ilifanyika Nanyuki Nchini Kenya.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan (watatu kulia) akiwa kwenye picha ya pamoja na Waheshimiwa Wabunge na watendaji wa Taasisi zingine za Jumuiya ya Afrika Mashariki mara baaada ya ufunguzi wa semina ya 9 ya kuimarisha uhusiano (Nanyuki 9) kati ya Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki na Wabunge kutoka Nchi Wanachama.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluh Hassan akitoa hotuba ya Ufunguzi wa Semina ya 9 ya kuimarisha uhusiano (Nanyuki 9) kati ya Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki na Wabunge kutoka Nchi Wanachama.
Naibu Waziri Mhe. Dkt. Susan Kolimba akihutubia Waheshimiwa Wabunge kwenye Semina ya 9 ya kuimarisha uhusiano (Nanyuki 9) kati ya Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki na Wabunge kutoka Nchi Wanachama.
Spika wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki Mhe. Daniel Kidega akihutubia Wabunge katika Semina ya 9 ya kuimarisha uhusiano (Nanyuki 9) kati ya Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki na Wabunge kutoka Nchi Wanachama iliyofanyika ukumbi wa LAPF Towers Jijini Dar es Salaam Mchi 3, 2016.
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai akihutubia Waheshimiwa Wabunge kwenye Semina ya 9 ya kuimarisha uhusiano (Nanyuki 9) kati ya Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki na Wabunge kutoka Nchi Wanachama iliyofanyika jijini Dar es Salaam
Baadhi ya waheshimiwa Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Wabunge wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki wakiimba wimbo wa Taifa kabla ya ufunguzi wa Semina ya 9 ya kuimarisha uhusiano (Nanyuki 9) kati ya Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki na Wabunge kutoka Nchi Wanachama. Semina hii hufanyika kila mwaka kwa mzunguko katika Nchi Wanachama na kwa mara ya kwanza ilifanyika Nanyuki Nchini Kenya.
















Friday 4 March 2016

HABARI PICHA; UZINDUZI WA BARABARA YA ARUSHA-HOLILI-TAVETA-VOI

Baadhi ya Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki, wakiwa katika picha ya pamoja mbele ya vifaa vitakavyo tumika katika ujenzi wa barabara ya Arusha-Holili-Taveta-Voi Machi3, 2016
Baadhi ya Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki wakionesha furaha mara baada ya kukata utepe kuashiria uzinduzi wa ujenzi wa Barabara ya Arusha-Holili-Taveta-Voi Jijini Arusha Machi 23, 2016
Baadhi ya Wakuu wa Nchi Wanachama za Jumuiya ya Afrika Mashariki na Wawakilishi wa Wakuu wengine wakiwa katika picha ya pamoja na  viongozi mbalimbali kutoka Nchi wanachama mara baada ya Mkutano wa 17 wakaiwaida wa Wakuu hao uliofanyika Hoteli ya Ngurdoto Jijini Arusha Machi 2, 2016.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akimkaribisha Balozi wa Japan apande mti kwa niaba yake wakati wa uzinduzi wa barabara ya Arusha-holili-Taveta-Voi, Machi3, 2016 Tengeru Arusha
Waziri wa Masuala ya Afrika Mashariki wa Rwanda Mhe. Valentine Rugwabiza (kulia) na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Sudan Kusini (Kushoto) wakipanda miti kwenye uzinduzi wa barabara ya Arusha-holili-Taveta-Voi,  Machi 3, 2016 Tengeru Arusha.



















Tanzania Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa mara nyingine


Tanzania Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa mara nyingine

Katika Hoteli ya Ngurugoto Jijini Arusha Mkutano wa 17 wa Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki chini ya
Mhe. Rais John Pombe Magufuli akisisitiza jambo
Mwenyekiti Mhe. John Pombe Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Tanzania imeombwa na wakuu wa Nchi hizo kuendelea kushikilia kiti hicho kwa Mwaka mwingine.

Mkutano huo ambao ulikuwa wa kipekee kutokana na jinsi Mwenyekiti alivyoeendesha Mkutano, umejadili na kupitisha maamuzi mbalimbali, kati ya maamuzi hayo ni pamoja na kuchagua Katibu Mkuu mpya wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Mkutano huu kutokana na matakwa ya Mkataba wa Jumuiya unaoelekeza kuwa Katibu Mkuu wa Jumuiya atakaa na cheo hicho kwa kipindi cha Miaka mitano(5). 

Hivyo mkutano huu umemteua Bw. Liberat Mfumukeko kuwa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, madaraka hayo ataanza rasmi kuyatumikia tarehe 26 Aprili,2016 tarehe ambayo Katibu Mkuu wa sasa Dkt. Richard Sezibera atakuwa amemaliza kipindi chake.

Mkutano huu vilevile uliridhia maombi ya kujiunga na Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa Jamhuri ya Sudan Kusini, kuridhia kwa maombi haya kunafanya Jumuiya sasa kuwa na Nchi wanachama sita(6). Wakiongea kwa nyakati tofauti Wakuu hawa wa Nchi waliipongeza Nchi ya Sudan ya Kusini na kuwakaribisha katika Jumuiya. “Kila Nchi ina matatizo yake cha muhimu ni kuvumiliana na kuheshimiana ili tuweze kufikia lengo letu la kuwaletea Wanaafrika Mashariki maeendeleo, tunawakaribisha sana wenzetu kutoka Jamhuri ya Sudan, kujiunga kwa Sudan ya Kusini kunafanya Jumuiya kuwa na soko la watu zaidi ya Millioni 150” alisema Mwenyekiti.

Vilevile Mkutano huu umemteua Rais Msataafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Bw. Benjamini Wiliam Mkapa kuwa mwezeshaji wa mazungumzo ya kuleta amani Nchi ya Burundi.

Katika Mkutano huu Mwanafunzi Mtanzania Simon S. Mollel kutoka shule ya Sekondari ya Mzumbe alitunikiwa cheti na pesa taslimu kiasi cha Dola za Kimarekani 1500 kwa kuwa mshindi wa kwanza wa shindano la Insha la Jumuiya ya Afrika Mashariki, ushindi wa pili ulichukuliwa na mwanafunzi kutoka Kenya, wa tatu kutoka Rwanda, wanne kutoka Uganda na wa tano kutoka Burundi wote hawa walitunikiwa vyeti na pesa taslimu.

Wakuu wa Nchi katika mkutano huu walizindua Pasi mpya ya kusafiria ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, Pasi hii itakuwa ya kisasa kabisa na itaweza kutumika duniani kote, hivyo Wanaafrika Mashariki hawatalazimika kuwa na pasi nyingine, pasi hii inatarajiwa kuanza kutumika rasmi tarehe 1 Januari,2017.

Akiongea katika hotuba ya kufunga mkutano huu wa 17 wa Wakuu wa Nchi, Mwenyekiti wa Wakuu wa Nchi Mhe. John P. Magufuli, aliwasihi watendaji wa Secretariati ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kuzingatia matumizi mazuri ya pesa, aliwakumbusha kuwa hizi ni pesa za walipa kodi wa Afrika Mashariki hivyo ni vyema wakazingatia matumizi mazuri ya pesa, alitoa mfano wa matumizi ya ukumbi wa Hoteli ya Ngurudoto ambao ni ghali badala yake Mkutano huu ungeweza kufanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa ‘AICC’ ambao ni bei rahisi na ni Mkubwa. 

Akimalizia alisema “ tunatakiwa kuhakikisha kila mwanaafrika mashariki ananufaika na fursa za Jumuiya ya Afrika Mashariki, tusiwe Jumuiya ya kuwanyonya wananchi, yeyote ambaye ataenda kinyume na kuzingatia utaratibu huo sitasita kumripoti kwa Wakuu wa Nchi wenzangu ili atumbuliwe”.

Wakiongea kwa nyakati tofauti wakuu wa Nchi walimpongeza sana Mhe. John Pombe Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyeti wa Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa jinsi alivyoeendesha Mkutano huu kwa ustadi.

HABARI PICHA; MKUTANO WA 17 WA KAWAIDA WA WAKUU WA NCHI WANACHAMA ZA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI

Ujumbe wa  Tanzania ukifuatilia Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Kawaida wakifuatilia maendeleo ya Mkutano huo uliofanyika hivi karibuni jijini Arusha

Viongozi Wakuu wa Nchi Wanachama za Jumuiya ya Afrika Mashariki wakionesha mfano wa pasi za kusafiria ya Afrika Mashariki iliyozinduliwa Machi 2, 2016 Jijini Arusha.
Mshindi wa Insha Simon S. Mollel kutoka shule ya Sekondari Mzumbe akionesha pesa aliyopewa kama zawadi ya kuwa mshindi wa Kwanza Afrika Mashariki.
Mhe. Waziri Balozi Dkt. Augustine Mahiga (wakwanza kushoto) akimpongeza Katibu Mkuu mpya wa Sekretariati ya Jumuiya ya Afrika Mashariki mara baada ya kuapa.
Katibu Mkuu mpya wa Sekretariti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki Bw. Liberat Mfumukeko akiapa mara baada ya kuteuliwa kushisha nafasi hiyo.
Wajumbe wa mkutano kutoka Tanzania wakifuatilia Mkutano wa 17 Wakawaida wa Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika Jijini Arusha Machi 2, 2016.
Wajumbe wa Mkutano kutoka Tanzania wakifuatilia Mkutano wa 17 Wakawaida wa Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika Jijini Arusha Machi 2, 2016





















Wednesday 2 March 2016

WAZIRI AONGOZA MKUTANO WA 33 WA BARAZA LA MAWAZIRI LA AFRIKA MASHARIKI JIJINI ARUSHA

Mhe. Waziri Balozi Dkt. Mahiga ambaye ni mwenyekiti wa Barala la Mawaziri wa Afrika Mashariki akipokea ripoti ya Kamati ya Ukaguzi na Vihatarishi ya Mwaka 2014/15.
Mhe. Waziri Balozi Dkt. Augustine Mahiga (katikati) akimfuatilia Mwanasheria wa Jumuiya (hayupo pichani) wakati akiwasilisha taarifa kwenye Mkutano wa 33 wa Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya Afrika Mashariki, Kushoto ni Katibu Mkuu Balozi Dkt. Aziz P Mlima na Kulia ni Katibu Mkuu Sekretariati ya Jumuiya ya Afrika Mashariki Balozi Dkt. Richard Sezibera.
Baadhi ya Maafisa wa Tanzania wakifuatilia Mkutano
Mawaziri kutoka Tanzania (walioketi msatari wa mbele) wakifuatilia majadiliano yaliyokuwa yakiendelea katika Mkutano wa 33 wa Baraza la Mawaziri Jijini Arusha tarehe 29 Februari, 2016
Mhe.Waziri Balozi Dkt. Augustine Mahiga akijadiliana Jambo na Katibu Mkuu Balozi Dkt. Aziz P. Mlima, Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Dr. Richard Sezibera na Mkurugenzi Idara ya Siasa Ulinzi na Usalama- EAC Bw. Stephen Mbundi.