Monday 15 December 2014


Mh. Waziri Samuel Sitta (katikati) akipongezwa na Katibu Mkuu Bi. Joyce Mapunjo (kushoto) na Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala na Raslimali Watu Bi. Vedastina Justinian (kulia) baada ya kutunukiwa Nishani ya Daraja la pili ya Muungano na Mh. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika sherehe za Uhuru zilizofanyika Viwanja vya Ikulu Jijini Dar-es-Salaam 9/12/2014.








Mh. Waziri Samuel Sitta (katikati) akipongezwa na Katibu Mkuu Bi. Joyce Mapunjo (kushoto) na Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala na Raslimali Watu Bi. Vedastina Justinian (kulia) baada ya kutunukiwa Nishani ya Daraja la pili ya Muungano na Mh. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika sherehe za Uhuru zilizofanyika Viwanja vya Ikulu Jijini Dar-es-Salaam 9/12/2014.




Mh. Waziri Samuel Sitta akiwa katika Picha ya pamoja  na Mh. Rais Dk. Mrisho Jakaya Kikwete baada ya kutunukiwa Nishani ya Daraja la Pili ya Muungano wengine ni Viongozi wa Serikali, Viongozi Wastaafu, na Wengine waliotunukiwa Nishani hiyo katika Sherehe ya Uhuru iliyofanyika Ikulu Jijini Dar-es-Salaam 9/12/2014.

Thursday 27 November 2014




Naibu Waziri Mh. Dkt. Abdullah Juma Saadalla (Katikati), Katibu Mkuu Bi. Joyce Mapunjo (kushoto) na Waziri wa Biashara na Viwanda Zanzibar Mh. Nassor Ahmed Mazrui wakiongoza kikao cha majadiliano ya Nchi (Tanzania) leo Nov. 27,2014 jijini Nairobi, Kenya.

Naibu Waziri Mh. Dkt. Abdullah Juma Saadalla (Katikati), Katibu Mkuu Bi. Joyce Mapunjo (kushoto) na Waziri wa Biashara na Viwanda Zanzibar Mh. Nassor Ahmed Mazrui wakiongoza kikao cha majadiliano ya Nchi (Tanzania) leo Nov. 27,2014 jijini Nairobi, Kenya.


 Naibu Waziri Mh. Dkt. Abdullah Juma Saadalla (Katikati), Katibu Mkuu Bi. Joyce Mapunjo (kushoto) na Waziri wa Biashara na Viwanda Zanzibar Mh. Nassor Ahmed Mazrui wakiongoza kikao cha majadiliano ya Nchi (Tanzania) leo Nov. 27,2014 jijini Nairobi, Kenya.


Baadhi ya Wajumbe kutoka Tanzania wakiwa katika kikao cha Majadiliano ya ndani kabla ya kuanza kwa Mkutano wa Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya Afrika Mashariki Kesho Tarehe 28 Novemba, 2014 Jijini Nairobi, Kenya.


Baadhi ya Wajumbe kutoka Tanzania wakiwa katika kikao cha Majadiliano ya ndani kabla ya kuanza kwa Mkutano wa Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya Afrika Mashariki Kesho Tarehe 28 Novemba, 2014 Jijini Nairobi, Kenya.


 Baadhi ya Wajumbe kutoka Tanzania wakiwa katika kikao cha Majadiliano ya ndani kabla ya kuanza kwa Mkutano wa Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya Afrika Mashariki Kesho Tarehe 28 Novemba, 2014 Jijini Nairobi, Kenya.

 Baadhi ya Wajumbe kutoka Tanzania wakiwa katika kikao cha Majadiliano ya ndani kabla ya kuanza kwa Mkutano wa Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya Afrika Mashariki Kesho Tarehe 28 Novemba, 2014 Jijini Nairobi, Kenya.

Tuesday 21 October 2014





Naibu Waziri Dkt. Abdulla Juma Abdulla Saadala  mwenye kofia akioneshwa  namna Meli ya RV Jumuiya ya Ziwa Victoria Jijini Mwanza inavyofanya kazi, ikiwa katika mwendo ndani ya maji na nahodha wa meli hiyo  Captain Juma Nkwama Tarehe 14/10/2014.




Nahodha wa Meli ya RV Jumuiya Capt. Juma Nkwama akionesha furaha yake mara baada ya kumuonesha Naibu Waziri wa Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Abdulla Juma Abdulla Saadala namna Meli hiyo inavyofanyakazi ikiwa ndani ya maji Tarehe 14/10/2014.




Naibu Waziri wa Wizara  ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Abdulla Juma Abdulla Saadala akitiasaini kitabu cha mahudhurio ndani ya Meli ya RV Jumuiya katika Ziwa Victoria Jijini Mwanza Tarehe 14/10/2014.




Naibu Waziri, Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Abdulla Juma Abdulla Saadala akiendesha kikao ndani ya Meli ya RV Jumuiya ya Ziwa Victoria Jijini Mwanza Tarehe 14/10/2014.



Naibu Waziri Dkt. Abdulla Juma Abdulla Saadala akifafanua jambo ndani ya Meli ya RV Jumuiya ya Ziwa Victoria Jijini Mwanza katika kikao chake na nahodha wa Meli hiyo Peter Nkwama na Mhandisi wa meli hiyo Herman Bundala. Tarehe 14/10/2014.





Picha ya Meli ya RV Jumuiya, Meli ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Ziwa Victoria Jijini Mwanza.Tarehe 14/10/2014.








                                                                




Thursday 2 October 2014

VIKWAZO NANE VYA KIBIASHARA VYAPATIWA UFUMBUZI




Jumla ya vikwazo visivyo vya kiushuru (NTBs) nane vilivyoripotiwa vimepatiwa ufumbuzi katika Mkutano wa 15 wa kikanda uliofanyika Jijini Arusha kuanzia tarehe 25 - 27 Septemba, 2014.

Miongoni mwa vikwazo hivyo nane vilivotajwa kupatiwa ufumbuzi, vitatu kutoka Tanzania, kimoja kilihusu Nchi zote Wanachama na vinne Nchi nyingine wanachama.

Kwa upande wake Tanzania iliwasilisha taarifa ya kupunguzwa kwa idadi ya vituo vya mizani katika lango la kati ambavyo kwa sasa vimebaki sita kati ya 15 vya awali.

Hatua hii imechukuliwa sambamba na kuondolewa kwa vituo vya ukaguzi vya Polisi.

Katika mkutano huo Tanzania ilitoa taarifa ya kuongezwa kwa magari matano ya polisi kwa lengo la kuimarisha shughuli za doria katika lango la kati.

Aidha, katika mkutano huo vikwazo vingine vipya nane vya kibiashara viliripotiwa, kati ya hivyo vikwazo viwili viliripotiwa na Kenya dhidi ya Uganda, na Uganda dhidi ya Kenya iliripoti vikwazo vitano,na kikwazo kimoja kiliripotiwa na Tanzania dhidi ya Kenya.

Vikwazo vilivyoonekana kuleta utata Mkutano uliadhimia vilipelekwe kwenye Baraza la Mawaziri la Kisekta la Afrika Mashariki la Biashara, Viwanda, Fedha na Uwekezaji.

Miongoni mwa vikwazo vilivyotajwa kupelekwa kwenye Baraza la Mawaziri la Kisekta la Biashara, Viwanda, Fedha na Uwekezaji ni pamoja na kupima katika mizani magari matupu ya mizigo, Usajili wa bidhaa kutoka Mamlaka ya Dawa na Chakula, Mahitaji ya nembo au jina kutoka Mamlaka ya Dawa na Chakula na mahitaji ya chanjo ya homa ya manjano. 

Ilipendekezwa kuwa vikwazo vinavyolalamikiwa kutoka Mamlaka ya Dawa na Chakula vipelekwe Bodi ya Viwango ya Afrika Mashariki kwa ajili ya kupata maoni ya kitaalamu yatakayosaidia kupatikana kwa ufumbuzi.

Kwa Upande wake Serikali ya Tanzania imedhamiria kupunguza idadi ya vituo vya mizani kutoka vituo sita vya sasa mpaka vituo vitatu ifikapo June 2015.

Na Teodos Komba

Friday 12 September 2014

Mara Milele: Zaidi ya watu 300,000 wanatarajiwa kuhudhuria maadhimisho ya siku ya Mara (Mara Day Celebrations)

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Zaidi ya watu 300,000 wanatarajiwa kuhudhuria Sherehe za Maadhimisho ya Siku ya Mto Mara (Mara Day) yatakayofanyika katika uwanja wa Chuo Kikuu cha Maasai Mara,  Jimbo la Narok, Jamhuri ya  Kenya.

Maadhimisho ya siku ya Mara huadhimishwa kila mwaka kwa pamoja kati ya Tanzania na Kenya ambazo ni Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Hufanyika kwa pamoja ili kusherehekea mazingira ya Mto Mara na faida zake kwenye maisha yao.

Kwa mwaka huu Maadhimisho haya yamepangwa kufanyika tarehe 15th Septemba, 2014 na yatahudhuriwa na watu mashuhuri kutoka Tanzania na Kenya, wawakilishi kutoka serikali za majimbo ya Narok na Bomet, Mkoa wa Mara, Kamisheni ya Bonde la Ziwa Victoria(LVBC), Mashule, Sekta Binafsi na wawakilshi wa  asasi za Kijamii.

Tarehe “15th Septemba  ilikubaliwa na Baraza la Mawaziri la kumi(10) la Kisekta ya Bonde la Ziwa Victoria  Tarehe 4 Mei,2012 Kigali – Rwanda kuwa siku ya Mara yaani  ‘Mara Day’.

Maelekezo ya Baraza yanaongeza chachu kwenye utekelezaji wa sera ya usimamizi endelevu wa Mto Mara na Mazingira yake katika Bonde la Ziwa Victoria” na juhudi za Nchi za Tanzania na Kenya na serikali ya majimbo ya Narok,Bomet na Mkoa wa Mara hazina Budi kupongezwa kwa maandalizi ya siku hii yatakayopelekea kufanikisha maadhimisho haya.

Serikali za Tanzania na Kenya na Wadau wa maendeleo kama vile Shirika la Maendeleo la Kimarekani (USAID), World Wide for Nature (WWN), Nile Equatorial Lakes Subsidiary Action Program (NELSAP) na Sekta binafsi zimekuwa msaada mkubwa katika kuendeleza Mazingira ya Mto Mara.  

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Kenya wameahidi kushirikiana katika usimamizi endelevu wa Bonde la Mto Mara kama mazingira ya kiasili katika bonde la Ziwa Victoria linalochangia katika maendeleo endelevu ya kijamii, utunzaji mazingira na uhai wa uchumi wa nchi hizi. 

LVBC wanachukulia juhudi za ushirikiano wa Nchi hizi Wanachama kama hatua muhimu za kusimamia na kuendeleza rasilimali za jamii zilizozunguka maeneo haya ili kuweza kuchangia katika agenda za mtangamano wa Afrika Mashariki.   

Sekta binafsi na Asasi za Kijamii zinazozunguka jamii hizi sio tu kushiriki katika siku ya Mara bali kushiriki kikamilifu katika usimamizi endelevu wa mto Mara kwa kuwa maisha ya mamilioni ya watu na viumbe mbalimbali vya Hifadhi maarufu duniani ya Serengeti na mbuga ya Maasai Mara yanategemea ustawi wa Mazingira haya.

Kauli mbiu ya Maadhimisho ya mwaka huu ni “Mara Milele” na maadhimisho haya yanafanyika kipindi hiki muafaka ambacho uhamaji mkubwa wa Nyumbu na Wanyama wengine, ambapo inakadiriwa jumla ya Nyumbu milioni mbili(2) wanahama kutoka mbuga ya Serengeti- Tanzania kwenda mbuga ya Maasai – Mara Kenya kwa kipindi cha Julai mpaka Octoba kila Mwaka. Uhamaji huu ni kati ya Maajabu saba mapya ya Dunia.

Maadhimisho ya tatu(3) ya siku ya Mto Mara  yatatanguliwa na mkutano na vyombo vya habari, kupanda mti, michezo mbalimbali na shughuli nyingine ili kufanikisha maadhimisho haya. Matukio haya yatafanyika kama sehemu ya kuadhimisha Mto Mara kama rasilimali ya kikanda kwa maendeleo endelevu ya Bonde la Ziwa Victoria na kuongeza uelewa kwa wadau kwenye changamoto na umuhimu wa bonde la Mto Mara. 

Maazimisho haya ya Mto Mara yanalenga kujenga uelewa wa ekologia Mto huu kama rasilimali ya pamoja ya kikanda baina ya Nchi hizi mbili kwa kuwezesha wadau wa Mto mara umuhimu wa utunzaji bonde la mto Mara na viumbe vilivyomo kwa maendeleo ya Jamii zinazozunguka maeneo haya na Taifa kwa Ujumla.
    
“Maadhimisho ya Mto Mara yanapelekea mwonekano wa  mali asili zilizoko katika ukanada wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na umuhimu uliopo kwenye maliasili hii kwa maisha ya viumbe na uchumi wa Nchi hizi mbili.


IMETOLEWA NA WIZARA YA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI

Thursday 28 August 2014





Spika wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki Dkt. Margaret Zziwa akizungumza kwenye ufunguzi wa bunge hilo.
3. Spika wa Bunge la Tanzania Anne Makinda (kushoto) akiwa na Spika wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki Dkt. Margaret Zziwa wakati wa ufunguzi wa vikao vya bunge hilo kwenye ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam 27August, 2014.




Spika wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki Dkt. Margaret Zziwa akizungumza kwenye ufunguzi wa bunge hilo.
3. Spika wa Bunge la Tanzania Anne Makinda (kushoto) akiwa na Spika wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki Dkt. Margaret Zziwa wakati wa ufunguzi wa vikao vya bunge hilo kwenye ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam 27August, 2014.


Spika wa Bunge la Tanzania Anne Makinda akihutubia Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki (EALA) la kwanza kufanyika Dar es Salaam, tangu kuanza kwa utaratibu wa kufanyika kwa bunge hilo kwa mzunguko kwa kila nchi mwanachama wa Jumuiya. 

                                                     

Naibu Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki wa Tanzania Dkt. Abdullah Juma Abdullah  Saadalla (wa pili kushoto), akifuatilia ufunguzi wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki.Kulia ni Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri wa Afrika Mashariki, Phyllis Kandie  (Waziri kutoka Kenya) Shem Bagaine (Waziri kutoka Uganda), Leontine Nzeyimana (Waziri kutoka Burundi), Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Richard Sezibera na kushoto ni Mwanasheria Mkuu wa Jumuiya hiyo  Wilbert Kaahwa.

                                                            



Wabunge wa Bunge la Jumuiya ya Afrika  Mashariki (EALA) wakiwa katika picha ya pamoja na Spika wa Bunge hilo Dkt. Margaret Zziwa (wa nne kutoka kulia waliokaa) na Spika wa Bunge la Tanzania Anne Makinda, mara baada ya ufunguzi wa bunge hilo.


                                                         

Friday 15 August 2014

UFUNGUZI NA UZINDUZI WA MAONYESHO YA WAJASILIA MALI NA KIWANDA CHA SMOKE HOUSE STORE LIMITED MJINI BAGAMOYO

Katibu Mkuu wa Wizara ya ushirikiano wa Afrika Mashariki Bi Joyce Mapunjo akihutubia Wajasilia Mali wadogo mjini Bagamoyo wakati wa Ufunguzi wa Maonesho hayo yaliyoanza tarehe 14/8/2014.


Katibu Mkuu Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki (kulia) Bi Joyce Mapunjo akitembelea moja ya banda la mjasiliamali katika maonyesho ya wajasilia mali  mjini Bagamoyo mara baada ya kufungua maonesho hayo.
                                                                      

                                                                             
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bi Joyce Mapunjo akikata utepe kufungua kiwanda cha  kusindika Mvinyo utokanao na mmea wa Rozera  cha SMOKE HOUSE STORE LIMITED kinacho milikiwa na Bi Teddy Devis kilichopo Mkoa wa Pwani Wilaya ya Bagamoyo. 



Katibu Mkuu Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki Ndugu Bi. Joyce Mapunjo akipewa maelekezo na mmoja wa wajasilia mali alipo tembelea banda hilo.                                                                       


Wednesday 13 August 2014

Tanzania yaridhia Itifaki ya Umoja wa Fedha

Tanzania yaridhia Itifaki ya Umoja wa Fedha

Tanzania imeridhia rasmi Itifaki ya Umoja wa Fedha ambayo ni sheria muhimu katika utekelezaji wa hatua ya tatu ya Mtangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Itifaki hiyo iliridhiwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  tarehe 25 Juni 2014.
Itifaki ya Umoja wa Fedha ilisainiwa na Wakuu Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki Novemba 30, 2013 Jijini Kampala, Uganda wakati wa Mkutano wa 15 wa Kilele wa Wakuu wa Nchi hizo. Baada ya kusainiwa na Wakuu wa Nchi, Nchi wanachama zilitakiwa ziwe zimeridhia Itifaki hiyo ifikapo Julai 1, 2014 ili kuruhusu kuanza kwa utekelezaji wake. Baada ya kuridhiwa kwa Itifaki, Nchi wanachama zitatakiwa kufuata mpango mkakati wa utekelezaji ambao umeelezwa bayana kwenye Itifaki hiyo.
Utekelezaji wa Itifaki ya Umoja wa Fedha utapelekea Nchi wanachama yaani Burundi, Kenya, Rwanda, Tanzania na Uganda kuwa na sarafu moja ifikapo mwaka 2024. Ili kufikia hatua ya kuwa na sarafu moja mwaka 2024 baadhi ya mambo muhimu yanayotakiwa kufanyika ni pamoja na uanzishwaji wa Taasisi za Kifedha. Taasisi hizo ni pamoja na Taasisi ya Fedha ya Afrika Mashariki (ambayo baadaye itakua Benki Kuu ya Afrika Mashariki), Taasi ya Takwimu ya Afrika Mashariki, Tume ya Usimamizi, Ufuatiliaji na Udhibiti na Tume ya Huduma za Kifedha ya Afrika Mashariki. ,
Utekelezaji wa Itifaki utahusisha pia uhuishaji wa sera zao za kifedha zikiwemo za kubadilisha fedha, sera za malipo kupitia benki, sera zinazohusu uzalishaji na usambazaji wa takwimu na sera za masoko ya fedha.
Izingatiwe kuwa, kabla ya kuingia kwenye Sarafu moja mwaka 2024, nchi wanachama zitatakiwa kukidhi vigezo vya Muunganiko wa uchumi mpana (Microeconomic Convergence Criteria) vilivyowekwa ambavyo ni pamoja na:
        i.            kuwa na mfumuko wa bei usiozidi 8%;
      ii.            Kuwa na nakisi ya Bajeti isiyozidi 3% (pamoja na misaada);
    iii.            Kuwa na deni la taifa lisilozidi 50% ya Pato la Taifa;
  iv.            Kuwa na akiba ya fedha za kigeni ambazo zinatosheleza manunuzi ya bidhaa kutoka nje kwa kipindi cha miezi minne na nusu.
Vigezo hivyo vinatakiwa kutekelezwa kwa kipindi cha miaka mitatu mfululizo kukaribia 2024. Kama kutakua angalau na nchi tatu za Jumuiya zitakazoweza kufikia vigezo hivyo basi zitaweza kuanza kutumia sarafu moja.
Umoja wa Fedha ni hatua ya tatu ya Mtangamano wa Afrika Mashariki baada ya hatua za awali, Umoja wa Forodha (2005) na Soko la Pamoja (2010) kutekelezwa. Hata hivyo ili hatua ya Umoja wa Fedha iweze kufanikiwa inategemea utekelezaji wa hatua za awali za mtangamano na ushiriki wa wananchi katika kuzitumia fursa zitokanazo na mtangamano. Wizara inawahamasisha Watanzania kutumia fursa mbalimbali zitokanazo na Umoja wa Forodha na Soko la Pamoja.

Maonesho ya Juakali/NguvuKazi ni zaidi ya kuuza bidhaa

Kamati ya maandalizi ya maonesho ya 15 ya Juakali/Nguvukazi yakutana Jijini Kigali-Rwanda, mkutano huu ulioanza tarehe 30 Julai-August 1, 2014 katika ukumbi wa sports view hotel Kigali-Rwanda, lengo kuu la mkutano huu ikiwa ni kuandaa maonesho ya 15 ya Juakali/Nguvukazi yanayotarajiwa kuanza tarehe 1-7 Disemba,2014 katika Viwanja vya Gikondo-Rwanda.
Akifungua mkutano huu mwenyekiti Bi. Gladys Kinyuah kutoka Kenya alisema lengo kuu la maonesho haya si wajasiliamali kuuza bidhaa zao tu bali ni uwanja wa kubadilishana technologia, uzoefu na masoko, “wakati umefika sasa tuwaambie wajasiliamali wetu tunapofanya maonesho haya si kwenda kuuza bidhaa tu bali ni kutafuta masoko na kubadilishana ujuzi na technologia mpya kutoka kwa wenzetu”. Akifafanua Bi Gladys alitoa mfano wa Nchi zilizoshamiri kiuchumi kutokana na mchango wa sekta isiyo rasimi, nchi kama Marekani,Japan na Malasia wajasiliamali wana mchango mkubwa kwa kukuza uchumi wa Nchi hizo, mfano Japan sekta isiyo rasmi inachangia 80% ya uchumi wa nchi hiyo na hii ni kutokana na Nchi hiyo kuithamini na kuipa kipao mbele sekta hii muhimu.
Kamati ya maandalizi imekubaliana kwa mwaka huu maonesho haya yawe zaidi katika kumsaidia mjasiliamali kujua jinsi ya kutafuta masoko, kunadi bidhaa zake na kuhakikisha wanazingatia viwango ambavyo vitawawezesha kuuza bidhaa zao ndani ya Nchi za Afrika Mashariki na kwenye masoko ya Kimataifa.
 Ili kuwapa uwezo wajasiliamali wa Juakali/Nguvukazi kamati ya Maandalizi imekubaliana kutakuwa na kongamano la siku mbili litakalofanyika tarehe 1 na 3 Disemba, 2014 kwenye viwanja vya maonesho Rwanda ili kuweza kutoa elimu ya masoko na taratibu nyingine kwa wajasiliamali na kushirikishana shuhuda za wajasiliamali waliofanikiwa kwa kupitia maonesho ya Juakali, elimu hiyo itatolewa na wataalamu wa masoko kwa njia ya kuwasilisha na majadiliano.
Takwimu za ajira zinaonesha 80% ya ajira katika Nchi za Afrika Mashariki zianatoka katika sekta isiyo rasimi (MSEs), wakati umefika sasa sekta hii muhimu kwa Nchi za Afrika Mashariki kuaangaliwa kwa jicho la tatu.
Maonesho ya JuaKali/NguvuKazi ni maonesho yanayohusisha wajasiliamali wadogo kutoka Nchi za Afrika Mashariki, maonesho haya hufanyika kila mwisho wa mwaka kwa utaratibu wa mzunguko kwa kila Nchi mwanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kuandaa maonesho hayo. Maonesho haya yalianza tangu mwaka 1999 ikiwa ni mawazo ya wakuu wa Nchi waazilishi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki yaani Tanzania, Kenya na Uganda na baadae Rwanda na Burundi kujiunga, Mwaka huu maonesho haya yanatimiza miaka 15.
Wajasiliamali wanahimizwa kuhakikisha wanaboresha biashara zao hasa katika ufungaji wa biashara zao (Packaging) na kuonesha ubunifu wa hali ya juu ili kuweza kuipa thamani bidhaa na kuwezesha bidhaa hizi kuuzwa hata kwenye masoko ya Kimataifa, kwani kuna bidhaa nyingi nzuri zinazozalishwa na wajasiliamali wadogo ila huwa zinapoteza sifa kwa masoko ya nje sababu ya kukosa baadhi ya vigezo, hivyo ni vyema tukahakikisha tunapambana na changamoto hizo kwa kufuata taratibu zote na kuwa wabunifu ili tuweze kukuza uchumi wetu na kupunguza tatizo la ajira hasa kwa vijana.

Tuesday 12 August 2014

Tarime farmers say 'enough is enough' to crop buyers from Kenya

Mzee Isaac Nyangi (left) at MEAC office in Dar es Salaam when he paid a visit to learn about the procedures for exporting crops to Kenya in July 2014. Right is the author of  this article.

MZEE Isaac Nyangi (65) from Tarime District in Mara Region came to Dar es Salaam recently to enquire with the Ministry of East African Cooperation the procedures of exporting farm produces to Kenya after decades of exploitation by buyers from the neighboring country.

Nyangi who represents members of NEHO association of elder farmers above 60 years, says enough is enough after discovering that a bag of sweet potatoes, which they have been selling for Tsh. 40,000 per 100 kilos bag at farm get price, it actually fetches Tsh. 160,000 in Kenya.

“We have been exploited for so long by smugglers from Kenya now we want to know what procedures are so that we can export ourselves to Kenya,” says Mzee Nyangi who is a retired Aviation Security Officer and a leader of NEHO.

He says his association has decided to come clean after many years of selling crops to buyers who have been using informal routes to cross the borders in order to smuggle goods to the neighboring East African Community’s (EAC) partner country.
Since April this year NEHO Association embarked on productions of sweet potatoes after they failed to excel in production of Maize and Paprica due to crop diseases.
“We expect to harvest 300 bags this year and sell it to Kenya. We are even targeting UN refugee camps in Kenya but we cannot succeed unless we formalize our way of doing trade,” says Nyangi who used members’ donations to get fare for Dar es Salaam visit.

According to Mzee Nyangi, many farmers are afraid to cross formal border of Sirari because of bureaucracy at border and ignorance of procedures.

During 2 hours discussions with Ministry Staff, Nyangi ended up with a huge smile and became more optimistic about their trade because he was taken through all the procedures for exporting or importing in the EAC region.

He was also given various Swahili publications written in a simplified way so that he can share with colleagues when he goes back to Tarime. He was commended for the initiative and encouraged to motivate others to cross the Sirari border themselves in order to fetch better prices.

In addition Mr Nyangi was given a hotline number which he could use to report any barrier they will encounter via short message services (SMS) by writing word NTB (space) problem send to 15539. The NTBs SMS and Online Reporting and Monitoring system is hosted at Tanzania Chamber of Commerce Industry and Agriculture (TCCIA).The system supported by Trade mark East Africa (TMEA) has been able to capture several NTBs some of which are resolved and some are at different levels of discussion for resolution.

According to EAC agreed import/export procedures, traders are required to fill in a Certificate of Origin which authenticates the origin of goods. For traders with goods valued at $2000 and below they can obtain the simplified certificates at the borders.
Traders with goods valued above $2000 they need to use Clearing and Forwarding agents to fill the certificates of origin which can be obtained at Tanzania Chamber of Commerce Industry and Agriculture’s (TCCIA) offices across the country. TCCIA has recently introduced an Electronic certificate of Origin through which exporters can apply the Certificate of origin Online and therefore reducing the cost of doing business.  The system can be accessed via the following web link; http://www.tccia.com/eco/.

The cost of obtaining certificate of origin for goods destined to EAC member states is just Tsh. 5,000 and goods are not subjected to import as long as they are accompanied with the certificate that proves the goods are originating from Tanzania.
During his visit to Dar es Salaam Mr. Nyangi used the opportunity to enquire the prices for sweet potatoes and he found out that a bag of 100 kilos was sold at 80,000, twice as much of the Tarime price.
He said it did not make business sense for them to bring their crops to Dar es Salaam because of the distance compared to Nairobi.
According to social economic data for Tarime, agriculture represents 85% of economic activities and annually the district harvests 14,539 tons of sweet potatoes.
Other popular crops  harvested include 43,151 tons of maize, 2,882 tons of beans, 12,169 tons of bananas, 5,076 tons of sorghum, 8,815 tons of rice, , 33,809 tons of cassava and 2730 tons  and coffee. Most of these crops are sold to neighboring Kenya.
Mzee Nyangi’s story is familiar in many parts of Tanzania especially in the border communities where by buyers from neighboring countries buy crops at cheaper prices and others go as far as buying crops while still in farm leaving farmers in a vicious cycle of poverty.

However, the construction of One Stop Border Posts (OSBPs) in all Tanzania major borders is likely to reduce bureaucratic procedures, corruption and cut cost for traders. This in turn will encourage more farmers such as Mzee Nyangi to use formal borders instead of the so called Panya routes.
Written by Faraja Mgwabati