Tuesday 19 April 2016

HABARI PICHA; RAIS WA SUDAN KUSINI MHE. SALVA KIIR ASAINI MKATABA WA KUJIUNGA NA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli na Rais wa Sudani Kusini Mhe. Salva Kiir (wakwanza kushoto) wakiwa na baadhi ya Viongozi wa Juu Serikalini na wawakilishi kutoka Nchi Wanachama za Jumuiya ya Afrika Mashariki. Wakwanza kulia ni Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Rais wa Sudan Kusini Mhe. Salva Kiir mara baada ya kuwasili Jijini Dar es Salaam
Rais wa Sudan Kusini Mhe. Salva Kiir akisaini Mkataba wa  kujiunga na Jumuiya ya Afrika Mashariki, tukio hili lilifanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa Mhe. Susan Kolimba (katikati)  akiwa katika zoezi la kihistoria wakati Rais wa Sudani Kusini Mhe. Salva Kiir akisaini mkataba wa kujiunga na Jumuiya ya Afrika Mashariki, zoezi lililofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaa. Kulia ni Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Prof. Makame Mbarawa         

No comments:

Post a Comment