Monday 29 February 2016

HABARI PICHA; UZINDUZI WA KITUO CHA UTOAJI HUDUMA KWA PAMOJA MPAKANI HOLILI (OSBP)

Mhe. Waziri Balozi Dkt. Mahiga (wakwanza kushoto) akikata utepe wa kuashiria kufunguliwa rasmi kwa Jengo la OSBP la Holili.
Mhe. Waziri Balozi Dkt. Mahiga na Waziri wa Masuala ya Afrika Mashariki wa Kenya Mhe. Phillis Kandie (katikati) wakiwa katika picha ya pamoja  na viongozi wengine kutoka Nchi Wanachama za Jumuiya ya Afrika Mashariki 
Mhe. Waziri (katikati) akitembelea Jengo la OSBP kwa upande wa Kenya Taveta ambapo alifanya uzinduzi rasmi wa Jengo hilo.
Mhe. Waziri akitoa hotuba ya Ufunguzi wa Jengo.
Mhe.Waziri wa tatu kutoka kushoto akifuatiwa na Waziri wa Kenya anayesimamia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Phillis Kandie wakielekea upande wa Tanzania Holili kutoka Taveta kwa ajili ya ufunguzi rasmi wa Jengo la OSBP la Holili, wengine katibu mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Dr. Richard Sezibera kushoto kwa Mhe. Waziri.
Mhe. Waziri  Balozi Dkt. Augustine Mahiga (mwenye kipaza sauti mkononi) akizingumza na vyombo vya habari baada ya uzinduzi wa kituo cha utoaji huduma kwa pamoja (OSBP) cha Holili, Kulia ni Waziri wa Masuala ya Afrika Mashariki wa Kenya Bi. Kandie.
Mhe. Waziri Balozi Dkt. Augustine Mahiga akisalimiana na Waziri wa Masuala ya Afrika Mashariki wa Nchini Kenya Bibi Phillis Kandie walipo kutana Jijini Arusha kabla ya uzinduzi wa Kituo cha kutoa Huduma kwa Pamoja Mpakani (OSBP) Holili.
Mhe. Waziri Balozi Dkt. Mahiga na Waziri wa Masuala ya Afrika Mashariki wa Nchini Kenya Mhe. Phillis Kandie wakijadili jambo.

No comments:

Post a Comment